💃🎤 Paroles de chanson Française et Internationnales 🎤💃

 A   B   C   D   E   F   G   H   I   J   K   L   M   N   O   P   Q   R   S   T   U   V   W   X   Y   Z   0   1   2   3   4   5   6   7   8   9 
Artiste : Aslay
Titre : Sawa
Umechezea kamari moyo wangu
Umezitia dosari hisia zangu
Sinuni sicheki nalia na Mungu wangu
Nasepa na kufuli ghetto kwangu
Milango iko wazi

Najuta kukujua yoyo
Umeniacha na simanzi
Natetema naungua mgongo
Wapi mapaparazi

Wanaotaka kunijua yoyo
Umeniachia shazi
Na watoto wanalia nyumbani

Umenipa funzo
Mapenzi yamenikong´ota
Umeivunja nguzo
Leo nyumba inabomoka

Basi sawa, sawa sawa
Yatapita haya, sawa sawa
Oh sio vibaya, sawa sawa

Kidole kimoja kuvunja chawa, sawa sawa

Nikawa najipa moyo
Utarudi hata kesho
Mwenzangu ukaniona kituko
Kichekesho

Mfupa kumpa kibogoyo
Sawa ka unampa mateso
Ila na we kumbuka
Kuna aliyeona kesho, sawa

Umeniacha gizani mama
Alafu mbele sioni mama
Hivi nilie na nani mama
Maana naumia moyonii

Umenipa funzo

Mapenzi yamenikong´ota
Umeivunja nguzo
Leo nyumba inabomoka

Basi sawa, sawa sawa
Yatapita haya, sawa sawa
Oh sio vibaya, sawa sawa
Kidole kimoja kuvunja chawa, sawa sawa

We mchuchu nichukie, sawa sawa
Nitakuja nitulie, sawa sawa
We si ndege nidonyoe, sawa sawa
Makusudi nikomoe, sawa sawa