đŸ’ƒđŸŽ€ Paroles de chanson Française et Internationnales đŸŽ€đŸ’ƒ

 A   B   C   D   E   F   G   H   I   J   K   L   M   N   O   P   Q   R   S   T   U   V   W   X   Y   Z   0   1   2   3   4   5   6   7   8   9 
Artiste : Best Naso
Titre : Mwambie
Maringo na kiburi na dharau
Ukanifanya naimba
Mwambie sina raha
Ana ponzi mashonzi ila ye ndo anayenifaa
Shemela ye ki ukweli nampenda

Nikimkosa mi nitachizi
Mwambie tena tena tena mwambie
Shemela
Mwambie tena tena tena mwambie

Endapo akitaka gari akitaka nyumba
Mwambie uwezo sina
Tena mwambie mi niko tayari kutoa mahari
Ili nimuoe mazima

Nenda mwambie wenye pesa hawawezi mpenda
Akisha wapa watapotea
Tena mwambie asiache kujichunga
Na dua njema namuombea

Mwambie mi sitaki anichunie moyo wangu uumie
Daktari wangu ni yeye
Tena mwambie mi niko tayari

Kutoa mahari ili nimuoe mazima

Mwambie sina raha bila yeye
Nitaiaga dunia bila yeye
Mwambie sina raha bila yeye
Mwenzio sijiwezi bila yeye

Mwambie sina raha napenda cheko lake
Ucheshi mashallah
Mwambie sina raha mateso naumia eeh
Mwambie sina raha

Ni bora angekwenda kwa mganga
Huenda ningejua ameniroga
Kuliko visa anavyofanya
Ananikimbia akiniona

Ukimuona muulize au anataka nijiue

Mwambie aje ghetto anitulize
Mi mbona sina mwingine
Mwambie tutaenda kwao mi sina mashaka
Na sitamchezea aondoe shaka

Nenda mwambie wenye pesa hawawezi mpenda
Akisha wapa watapotea
Tena mwambie asiache kujichunga
Na dua njema namuombea

Mwambie sina raha bila yeye
Nitaiaga dunia bila yeye
Mwambie sina raha bila yeye
Mwenzio sijiwezi bila yeye

Mwambie sina raha napenda cheko lake
Ucheshi mashallah
Mwambie sina raha mateso naumia eeh

Mwambie sina raha, mwambie sina raha
Mwambie sina raha, mwambie sina raha