đŸ’ƒđŸŽ€ Paroles de chanson Française et Internationnales đŸŽ€đŸ’ƒ

 A   B   C   D   E   F   G   H   I   J   K   L   M   N   O   P   Q   R   S   T   U   V   W   X   Y   Z   0   1   2   3   4   5   6   7   8   9 
Artiste : Rose Muhando
Titre : Bado
Niiii, niiini, niii?
Niiii, niiini, niii?
Je nataka kuwa na nini?
Nauliza mnataka kuwa na nini?
Wasomi mnataka kuwa na nini?

Kanisa linataka kuwa na nini?
Ndipo mjue yametimia

Dunia hey, kama kulemewa
Imelema sana
Dunia hey, kama kuanguka
Imeanguka sana

Hivi mnataka kuwa na nini?
Ndipo mjue yametimia
Dunia inataka kuwa na nini?
Ndipo mjue Mungu anasema

Ona akili za wenye akili
Zimefika kikomo jamani
Maarifa ya wenye akili
Yameshindwa kabisa
Hekima ya wenye hekima haisaidii kitu

Hivi mnataka kuwa na nini?
Nauliza mnataka muone nini?
Ndivyo mjue Mungu anasema

Bado, bado, bado bado bado
Kama ni mapito, bado bado
Kama ni magonjwa, bado bado
Kama timbwili timbwili, bado na bado
Kama ni heka heka, bado bado
Msishangazwe na ya leo, bado bado

Baragumu ya kwanza imekwisha kupigwa
Dunia ijipange
Baragumu ya kwanza imekwisha kulia
Kanisa lijipange
Na hapa ndipo penye imani na subira
Ya watakatifu wajipange

Wenye masikio na wasikie neno hili
Roho asema mjipange
Na bado, bado, bado ni ishara tu

Basi inueni macho yenu
Tazama vilele vimeinama
Wafalme wamechanganyikiwa
Wenye akili hawana la kufanya
Manabii maono yamekoma
Ufunuo maono yamekoma
Ayaa sasa dunia yote mikono juu
Semeni Mungu pekee ndiye Bwana

Basi inueni macho yenu
Tazama vilele vimeinama
Wafalme wamechanganyikiwa
Wenye akili hawana la kufanya
Manabii maono yamekoma

Ufunuo maono yamekoma, bado

Nani basi asimame, mbele za Mungu aseme
Alete moja nyingine ashindane na Mungu tuone

Maneno ya Mungu kamwe hayatapita
Nasema mjipange
Kengele ya hatari imeshakwisha kulia
Nasema mjipange
Bado, bado, bado ni ishara tu

Bado, bado, bado bado bado
Na magonjwa bado, bado bado bado
Na shida bado, bado bado bado
Njaa na matetemeko, bado bado bado
Msishangazwe na ya leo, bado bado bado
Msisitishwe na ya leo, bado bado bado
Ah nasema bado, bado bado bado

Uwiii, bado bado bado